Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Featured Image

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.

Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.

Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.

Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.

Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

Baba yetu… …..Salamu Maria….…Atukuzwe Baba………

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Anthony Kariuki (Guest) on September 12, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joseph Kawawa (Guest) on September 4, 2017

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Nancy Kabura (Guest) on July 12, 2017

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Chris Okello (Guest) on March 29, 2017

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Joseph Kitine (Guest) on March 21, 2017

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Benjamin Masanja (Guest) on March 14, 2017

Mwamini Bwana; anajua njia

Janet Sumari (Guest) on January 10, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Simon Kiprono (Guest) on December 30, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Janet Mwikali (Guest) on July 26, 2016

Rehema zake hudumu milele

Grace Mushi (Guest) on July 11, 2016

πŸ™πŸ™πŸ™

James Kawawa (Guest) on May 7, 2016

Sifa kwa Bwana!

Charles Mboje (Guest) on March 3, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Joseph Kitine (Guest) on October 19, 2015

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Grace Majaliwa (Guest) on October 3, 2015

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Ann Awino (Guest) on October 2, 2015

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Nuru (Guest) on September 8, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

David Musyoka (Guest) on August 15, 2015

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Grace Mushi (Guest) on July 22, 2015

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Grace Minja (Guest) on June 17, 2015

Baraka kwako na familia yako.

Elizabeth Malima (Guest) on June 10, 2015

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Alex Nyamweya (Guest) on May 18, 2015

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Elizabeth Malima (Guest) on May 16, 2015

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Joseph Mallya (Guest) on April 3, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Related Posts

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuhesh... Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)