Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Jinsi ya kuandaa Muhogo, Samaki Wa Kuchoma Na Bamia

Featured Image

Mahitaji

Mihongo 3 - 4

Tui - 1000 ml

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu maji kilokatwakatwa - 1

Nyanya mshumaa - 3-4

Pilipili mbichi ndefu - 2-3

Pilipili boga - 2

Namna Ya Kutayrisha Na Kupika

Menya mihogo kisha ikate kate vipande inchi tatu hadi nne, kila kipande kigawe kitoke vipanda vinne. Toa mzizi katikati
Osha mihogo ipange kwenye sufuria ya nafasi na yenye mfiniko, ili upate nafasi ya kutia viungo unavyoona pichani na utokotaji wa tui wahitaji nafasi.
Panga/tandaza kitunguu, nyanya mshumaa/tungule,pilipili mbichi na pilipili boga juu ya mihogo, tia chumvi na tui lote.
Funika sufuria kisha weka jikoni moto wa kiasi kuchemsha tui lipande juu. Hakikisha tui halifuriki na kumwagika kwa kuchungulia au kufunika nusu mfuniko
Kwa mda wa nusu saa hivi ukiona sasa tui linatokota chini chini fuinika mfiniko na upunguze moto mdogo kabisa tui likauke kidogo na liwe zito.
Toa muhogo moja ubonyeze ukiona umewiva zima jiko na wacha sufuria hapo kwa muda wa 10. Mihogo tayari kuliwa.

Kidokezo.

Tui lote huwa chini baada ya mihogo kuwiva unapopakuwa teka kutoka chini uweze kupata uzito wa tui umwagie juu.

Bamia/Mabenda

Bamia - robo kilo

Nyanya - 3

Kitunguu maji - 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au ilosagwa - 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo (tomato paste) - 1 kijiko cha supu

Mafuta - 150 ml

Chumvi -1 kijiko cha chai

Pilipili boga - 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Kata vichwa vya bamia kisha zikate kate mara mbili zikiwa kubwa, ikiwa ni ndogo mno haina lazima kuzikata osha tu uweke kando.
Katika sufuria, katakata kitunguu, nyanya, pilipili boga tia ndani viungo hivi ongeza chumvi mafuta, thomu na nyanya kop
Washa moto mdogo mdogo huku umefunika sufuria kwa muda wa dakika 20 kisha ukiona mboga zimeshika kutokota ongeza bamia koroga.
Tia maji 200ml wacha kwa muda wa dakika 15 kupikika tena, ukionja utamu wa mboga na chumvi, hakikisha bamia pia zimewiva. Tayari kuliwa.

Samaki Wa Kuchoma

Samaki (dorado) au mikizi au una - 2 wakubwa (fresh)

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au iliyosagwa 1 Β½ cha chai

Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayrisha Na Kuchoma

Safisha samaki vizuri mchane chane (slit) kwa ajili ya kuweka masala.
Changanya viungo vyote na chumvi samaki kisha paka katika samaki kote na ndani ya sehemu ulizochanachana. Mroweke kwa muda wa robo saa hivi.
Weka karatasi ya jalbosi (foil paper) katika treya ya oveni. Muweke samaki kisha mpike (grill) kwa moto wa juu achomeke hadi samaki agueke rangi na awive.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Viambaupishi Vya Masala

Nyama vipande - 3 LB

Mtindi - Β½ kopo

Kitunguu (thomu... Read More

Mapishi – Saladi ya Matunda

Mapishi – Saladi ya Matunda

Matunda ni mojawapo wa kundi la vyakula, ni muhimu sana kwa afya bora. Matunda yakitengenezwa viz... Read More

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Vidokezo vya kukusaidia ule mboga za majani zaidi

Ulaji wa mboga za majani ni muhimu kwa sababu zina vitamini na madini mengi na viwango vidogo vy... Read More

Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Ngogwe Na Bamia

Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Ngogwe Na Bamia

Viamba upishi

Ngogwe Β½ kg
Kitunguu 2
Bamia ΒΌ kg
Karoti 2
Mafuta vij... Read More

Mapishi ya Wali na kuku wa kienyeji

Mapishi ya Wali na kuku wa kienyeji

Mahitaji

Kuku wa kienyeji (boiler chicken 1)
Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyanya ya k... Read More

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mahitaji

Kunde (Ila mimi nilitumia Nigerian brown beans 1/2 kilo)
Vitunguu maji (oni... Read More

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

MAHITAJI

Mchele wa pishori (basmati) - 4

Nyama ya kuku bila mafupa - 1 Lb

Kam... Read More

Upishi wa Afya kwa Ajili ya Afya ya Moyo: Kitamu na Kilainishi

Upishi wa Afya kwa Ajili ya Afya ya Moyo: Kitamu na Kilainishi

Upishi wa Afya kwa Ajili ya Afya ya Moyo: Kitamu na Kilainishi πŸπŸ’šπŸŒ½

Leo, tutazungu... Read More

Jinsi ya kupika Eggchop

Jinsi ya kupika Eggchop

Mahitaji

Mayai yaliochemshwa 4
Nyama ya kusaga robo kilo
Kitunguu swaum
Ta... Read More

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 Vikombe

Dengu - 2 vikombe

Viazi - 3 vikubwaRead More

Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu

Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu

Mahitaji

Bamia (okra) 20
Nyanya chungu (garden eggs) 5
Magadi soda (Bicabonate ... Read More

Vidokezo 10 vya Vitafunio vya Afya kwa Watoto Wagumu Kula

Vidokezo 10 vya Vitafunio vya Afya kwa Watoto Wagumu Kula

Vidokezo 10 vya Vitafunio vya Afya kwa Watoto Wagumu Kula

Kama mzazi au mlezi, mara nyingi... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About