Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma Wa Tanduri

Featured Image

Mahitaji

Mchele - 4 vikombe

Kuku - 1

Vitunguu - 3

Nyanya/tungule - 4

Zabibu kavu - ยฝ kikombe

Tangawizi na kitunguu (thomu/galic) - 2 vijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Mtindi (yoghurt) - 2 kijiko cha supu

Masala ya tanduri - 2 vijiko vya supu

Pilipili manga - 1 kijiko cha chai

Hiliki - ยฝ kijiko cha chai

Mdalasini - kijiti kimoja

Ndimu - 3 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Zaafarani (saffron) - 1 kijiko cha chai

Mafuta - ยฝ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Kuku:

Baada ya kumsafisha kuku, mkate vipande vikubwa vikubwa kiasi upendavyo, muoshe mchuje atoke maji.
Katika bakuli, tia tangawizi, kitunguu thomu ilosagawa, pilipili mbichi ilosagwa, chumvi, ndimu, mtindi, masala ya tanduri na uchanganye vizuri, kisha mtie kuku na uchanganye tena na acha arowanike kwa muda wa kiasi saa au zaidi.
Panga kuku katika sinia ya kuchoma ndani ya oveni. Kisha mchome (grill) hadi awive, mtoe acha kando. Mwagia juu yake masala yatakayobakia katika sinia baada ya kumchoma.

Namna Ya Kutayarisha Masala Ya Nyanya:

Weka mafuta katika karai, tia vitunguu ulivyokatakata, kaanga hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya ulizokatakata, tia pilipili manga, hiliki, mdalasini, chumvi, na zabibu. Kaanga kidogo tu yakiwa tayari.

Namna Ya Kutayarisha Wali:

Osha na roweka mchele wa basmati.
Roweka zaafarani kwa maji ya moto kiasi robo kikombe weka kando.
Chemsha maji, tia chumvi, kisha tia mchele uive nusu kiini.
Mwaga maji uchuje mchele kisha rudisha katika sufuria au sinia ya foil. Nyunyizia zaafarini, na rudisha katika moto upike hadi uive kamili.
Epua, kisha pakua wali katika sahani au chombo upendacho, mwagia juu yake masala ya nyanya. Kisha weka vipande vya kuku ulivyochoma, biriani ikiwa tayari

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe

Sukari - 1 Kikombe

Baking powder 1 kijiko cha c... Read More

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Tambi

MAHITAJI

Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2

Siagi - 4 Vijiko vya supu

Maziwa ... Read More

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Vipimo

Ndizi mbichi - 10

Nyama - kilo 1

Nazi ya kopo - 1

Chumvi - 1 Kij... Read More

Mapishi ya Wali na kuku wa kienyeji

Mapishi ya Wali na kuku wa kienyeji

Mahitaji

Kuku wa kienyeji (boiler chicken 1)
Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyanya ya k... Read More

Mapishi ya Kachori

Mapishi ya Kachori

Mahitaji

Viazi mbatata (potato 4 vya wastani)
Nyama ya kusaga (mince beef 1 kikombe ... Read More

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

Namna ya kutengeneza Visheti Vya Nazi Na Njugu (Sudani)

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 mug za chai

Samli - ยฝ mug ya chai

Maziwa - 1ยผ mug ya ... Read More

Jinsi ya kutengeneza Keki Ya Mbegu Za Mchicha

Jinsi ya kutengeneza Keki Ya Mbegu Za Mchicha

Viamba upishi

Unga ngano vikombc 3
Unga mbegu za mchicha kikombe 1
Baking powde... Read More

Mapishi ya Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Mapishi ya Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Mahitaji

Mchele - 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) - Mug

Tuna... Read More

Mapishi ya Mihogo ya nazi na kuku

Mapishi ya Mihogo ya nazi na kuku

Mahitaji

Mihogo kilo 1
Kidali cha kuku 1 kikubwa
Nyanya 1 kubwa
Kitunguu m... Read More

Jinsi ya kupika Vileja Vya Tambi

Jinsi ya kupika Vileja Vya Tambi

Viambaupishi

Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2 Siagi 4 Vijiko vya supu Maziwa (condensed... Read More
Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mapishi ya Maini ya ng'ombe

Mahitaji

Maini (Cow liver) 1/4 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2
Nyanya (chopped ... Read More

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Mahitaji

Nyama Ya Mbuzi - 1 Kilo

Mchele - 4 Magi

Vitunguu - 3

Nyanya - ... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About