Dalili na matibabu ya tatizo la upungufu wa damu
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Upungufu wa damu ni tatizo linalosababishwa na kupoteza damu nyingi, kupungua kwa uzalishaji wa chembe hai za da damu na uharibifu wa chembe za damu kutokana na matatizo na magonjwa mbali mbali seli mundu, ujauzito, hedhi nzito, kurithi, magonjwa sugu na Lishe duni yenye ukosefu wa madini ya folic, chuma na vitamini B12.
Dalili
Dalili zifuatazo zinakuwezesha kutambua kama una tatizo la upungufu wa damu hivyo kukusaidia kuwahi hospitali au kubadili mfumo wa chakula ili kuepuka madhara makubwa ya baadae.
· Kushindwa kupumua vizuri
· Vidonda kwenye ulimi au mdomoni
· Sehemu nyeupe ya jicho kuwa bluu
· Ngozi kuwa na rangi ya kijivu
· Kucha kuwa dhaifu
· Kusikia hasira na kuhamasika haraka
· Kuchoka sana kuliko kawaida
· Maumivu makali ya kichwa
· Kupungua kwa uwezo wa kufikiria
· Kusikia kichwa chepesi pale unaposimama
· Miguu na mikono kuwa ya baridi sana
· Uchovu wa mara kwa mara
Matibabu.
Upungufu wa damu hutibiwa mapema kwa kubadili lishe pamoja na kuongeza lishe yenye vitamini C na B12 pamoja na madini ya Chuma kutokana na visababishi vya tatizo. Mara nyingine vidonge na sindano zenye lishe hizi huweza kutumika hosipitali na matibabu ya tatizo linalosababisha na iwapo mgonjwa yuko katika hali mahututi huweza kuongezewa damu.
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Mungu ameumba miti na mimea kwa ajili ya binadamu. Kila mti au mmea una makusudio yake. Mbuyu ni ...
Read More
Watu wengi hulitumia tunda la papai kwa sababu ya utamu wake. Hata hivyo mbali na kuwa na ladha n...
Read More
Tatizo la kukosa choo (constipation) ni tatizo ambalo limekuwa likiwakumba watu wengi sana katika du...
Read More
Kitaalamu chakula unachokula leo ndio kinaamua hali ya afya yako kwa siku za usoni. Na ni muhimu ...
Read More
Mshubiri au Aloe Vera kama ilivyozoeleka na namna nzuri kwa wale wote wanaotaka kubaki na ngozi ...
Read More
Naamini umeshawahi kusikia kuhusu changamoto ya uvimbe kwenye kizazi kwa Wanawake yaani Fibroids....
Read More
Kuamka asubuhi na mapema hupunguza uwezekano wa mwanamke kupata saratani ya matiti.
Kulinga...
Read More
Zabibu huweza kutumika kama tiba ya shinikizo la chini la damu kama ifuatavyo
Dawa nyingine madhubuti ya chunusi ni papai. Tunda hili ni moja ya matunda yanayotumika kwa ajili...
Read More
Leo tutaongelea mazoezi gani ya kawaida ambayo mama mjamzito anaweza kuendelea kuyafanya kila sik...
Read More
Siku zote sisi wanadamu huwa tunaambizana kuwa, kinga ni bora kuliko tiba, tukiwa na maana kwamba...
Read More
Pombe ni kinywaji kinachotumiwa na watu wengi pasipo hata kufahamu athari zake. Pombe ina athari ...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!