Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Haki zinazokiukwa iwapo mvulana au msichana wamelazimishwa kuoa au kuolewa

Haki zinazokiukwa iwapo mvulana au msichana wamelazimishwa kuoa au kuolewa

Nani na lini unaoa ni maamuzi yako binafsi wewe mwenyewe,
hata kama rafiki na wazazi wanakus... Read More

Je, ni kweli matumizi ya dawa za kulevya ni mojawapo ya sababu zinazochangia maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU)

Je, ni kweli matumizi ya dawa za kulevya ni mojawapo ya sababu zinazochangia maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU)

Dawa za kulevya zenyewe hazisababishi UKIMWI na magonjwa ya zinaa. Lakini utumiaji wa dawa za kul... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

H... Read More

Je, watu wanapendelea kujaribu kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kujaribu kufanya mapenzi?

Habari za leo wapendwa wasomaji! Leo, tunajadili kuhusu je, watu wanapendelea kujaribu kufanya ma... Read More

Ni katika umri gani vijana wana haki ya kujihusisha na mambo ya kujamiiana?

Ni katika umri gani vijana wana haki ya kujihusisha na mambo ya kujamiiana?

Kujamiiana ni uamuzi wa mtu binafsi. Ni uamuzi wako na hakuna
mtu yeyote mwenye haki ya kuku... Read More

Niende wapi kupima kama nina Virusi vya UKIMWI?

Niende wapi kupima kama nina Virusi vya UKIMWI?

Vituo vyenye utaalamu na katika hospitali i au Taasisis kama vile Shirika la Amref au CCBRT wana ... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano ya Wazi na Msichana Wako

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano ya Wazi na Msichana Wako

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano ya Wazi na Msichana Wako

Ndoa ni muunganiko wa wawili kuwa ki... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Mawazo yasiyofaa kuhusu Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Mawazo yasiyofaa kuhusu Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Mawazo yasiyofaa kuhusu Ngono? πŸ€”βœ‹

  1. Jua vipaumbele v... Read More

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Nikitumia nyembe kali au sindano pamoja na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI ninaweza kupata Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Ndiyo, unaweza kuambukizwa ukitumia nyembe kali au sindano kwa kuchangia pamoja na mtu mwenye vir... Read More

Kwa nini watu wengine hupenda kujamiiana na watu wa jinsi sawasawa? mapenzi ya jinsia moja

Kwa nini watu wengine hupenda kujamiiana na watu wa jinsi sawasawa? mapenzi ya jinsia moja

Ni vigumu kutoa jibu kamili kwa nini hisia hii i ii inatokea kwa watu wengine, kwa sababu wataala... Read More

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Jinsi ya Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono 😊😊😊

Karibu... Read More

Sheria kuhusu utoaji mimba

Sheria kuhusu utoaji mimba

Sheria kuhusu utoaji
mimba zinatofautiana
kati ya nchi na nchi. Hapa
Tanzania utoa... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About