Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Ushauri kwa mtu aliyebakwa

Ushauri kwa mtu aliyebakwa

Jambo la kwanza jaribu kumwondoa hofu mwathiriwa na
muliwaze maana amepata jambo la kutisha.... Read More

Je, mwanamke anajisikiaje akijamiiana na mwanaume aliyevaa kondomu au aliye β€œpeku”?

Je, mwanamke anajisikiaje akijamiiana na mwanaume aliyevaa kondomu au aliye β€œpeku”?

Hatuwezi kusema mwanamke husikia raha gani akijamiiana na mwanaume aliyevaa kondomu au na mwanaum... Read More

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Kufadhaika na Utendaji wa Ngono/Kufanya mapenzi

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Kufadhaika na Utendaji wa Ngono/Kufanya mapenzi

Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Kufadhaika na Utendaji wa Ngono/Kufanya Mapenzi 😊πŸ”₯

... Read More

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za kiutamaduni katika ngono/kufanya mapenzi? Swali hili linaweza kusababisha maj... Read More

Je, ni madhara gani atapata mama mjamzito endapo atajamiiana na mwenzi wake?

Je, ni madhara gani atapata mama mjamzito endapo atajamiiana na mwenzi wake?

Kama kati ya mwanamke na mwanaume hakuna mwenye magonjwa ya zinaa, hakuna madhara yoyote kwa mwan... Read More

Utoaji wa zawadi kwa kubadilishana na kujamiiana

Utoaji wa zawadi kwa kubadilishana na kujamiiana

Kutoa zawadi kwa mtu kwa kubadilishana ili kujamiiana
ni unyanyasaji mbaya. Iwapo mpokeaji w... Read More

Je, nikiambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI nifanye nini?

Je, nikiambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI nifanye nini?

Jambo la msingi ni kutokukata tamaa na kuwa na matumaini. Mara nyingine i inasaidia kama utakuwa ... Read More

Je, kuna umuhimu wa ngono/kufanya mapenzi unabadilika wakati wa mzunguko wa maisha?

Je, kuna umuhimu wa ngono/kufanya mapenzi unabadilika wakati wa mzunguko wa maisha?

Habari za leo wapenzi wangu! Nami nina furaha sana kuwa hapa leo kuongelea kuhusu swala la ngono ... Read More

Kutahiriwa kwa wanaume ni sawa na ukeketaji?

Kutahiriwa kwa wanaume ni sawa na ukeketaji?

Hapana. Ukeketaji na kutahiriwa kwa mwanaume havifanani.
Kama kutahiriwa kwa mwanamume ni sa... Read More

Je, ni kweli ukinywa maziwa baada ya kuvuta sigara huwezi kudhurika?

Je, ni kweli ukinywa maziwa baada ya kuvuta sigara huwezi kudhurika?

Hapana. Hii si kweli kwa sababu maziwa hayawezi kuondoa
uharibifu uliosababishwa na nikotini... Read More

Je, kuna umuhimu wa kufanya mazoezi ya kuboresha nguvu na stamina wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kufanya mazoezi ya kuboresha nguvu na stamina wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kufanya mazoezi ya kuboresha nguvu na stamina wakati wa ngono/kufanya mapenzi... Read More

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanaweza kuvumisha uongo wowote ili kupotosha
ukweli na kufanya mambo yao maovu wanayoy... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About