Nikitafuta rafiki kwa nia ya kuoana (mchumba), je ni sifa gani niangalie kwa msichana/mvulana?
Date: April 17, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Kuchagua mchumba ni moja ya maamuzi ambayo kijana anahitaji kuyafanya kwa uangalifu mkubwa sana. Kwa sababu huyo ndiye atakayekuwa mwenzi wake wa maisha. Katika kuchagua mchumba kila mtu ana mawazo yake kuhusiana na kilicho muhimu kuzingatiwa. Mara nyingi mhemuko una nguvu zaidi kuliko uamuzi wa kimantiki
Hata hivyo, vifuatavyo ni kati ya vigezo ambavyo vinaweza kuangaliwa:
β’ Chagua mtu anayekuheshimu wewe na wengine; Chagua mtu unayemwamini;
β’ Chagua mtu ambaye unaweza kuongea, kujadiliana, na kuhojiana naye kwa uwazi bila kugombana;
β’ Chagua mtu mwenye umri unaokaribiana na wa kwako;
β’ Chagua mtu anayependelea vile unavyopendelea;
β’ Chagua mtu ambaye ataelewa matatizo yako na yuko tayari kukusaidia kuyatatua; na
β’ Chagua mtu mwenye afya nzuri.
Hii inamaanisha pia kumpata mtu ambaye kabla ya kuanza kujaamiana naye, atakuwa tayari kwenda kupima kwa hiari kujua hali yake ya VVU na pia kuwa tayari kutumia kinga kwa maana ya kondomu hadi hapo mtakapojua hali zenu.
Wafahamishe wazazi wako mtu uliyemchagua kama mchumba na mtambulishe kwao i ili wamfahamu na yeye awafahamu wazazi wako. Wakati huohuo na wewe jaribu kuwafahamu wazazi wake. Usifanye uchumba wa haraka. Pata muda wa kutosha kumwelewa rafiki yako.
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Jinsi ya Kujifunza Kujiheshimu na Kuheshimu Wengine kuhusu Ngono ππ
Karibu sana kija...
Read More
Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Uaminifu kuhusu Ngono? π
Karibu kwa makala hii...
Read More
Ni imani na fikra potofu kwamba, ukinywa gongo au kuvuta
sigara kwa kiasi kidogo baada ya ch...
Read More
Wakati mwingine ni vigumu kusema hapana ukiwa na
maana ya hapana. Jaribu kuwa mpole na usiwe...
Read More
Kupata mazungumzo ya kuvutia kwa msichana unayempenda kunaweza kuwa changamoto kubwa kwa wanaume ...
Read More
Habari za leo wapenzi! Sijui kama umewahi kujiuliza kuhusu umuhimu wa usawa wa ngono/kufanya mape...
Read More
Leo tutazungumzia kuhusu imani za watu katika kuelewa na kuheshimu mipaka ya kimwili katika uhusi...
Read More
Watu wengi huwaona Albino kama watu tofauti na watu wengine
na kuwakwepa, wanaweza hata kuba...
Read More
Pamoja na matatizo ya kuona, ngozi ya Albino ni rahisi sana
kudhurika kwa mionzi ya jua. Hat...
Read More
Jinsi ya Kukabiliana na Hisia za Aibu Kuhusu Ngono π
Karibu vijana wenzangu! Leo, tutaj...
Read More
Kuzungumza na msichana kwa heshima na upendo ni kitu muhimu kwa kila kijana ambaye anataka kuwa n...
Read More
Je, kuna mambo mazuri na mabaya kuhusu ngono/kufanya mapenzi? Ndio, kuna mambo mengi sana ambayo ...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!