Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mambo ya Msingi kuyajua Ili uishi na watu vizuri

Featured Image

Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-
1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu, kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)
2. Usiwatendee wengine ubaya ukadhani kuwa utakuwa salama (ubaya hulipwa kwa ubaya, ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako)

3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti ukweli (pengine wapo wanadamu wanaopenda kuonekana wao wema kwa kuumiza wengine). Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.

4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji (tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya).

5. Usipande mbegu ya chuki na ubaya katika jamii unayoishi ukadhani itakuacha salama (chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.

6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe, mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.

6. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira. Kuongea sana kunapoteza busara.

7. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.

8. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile, ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri.

9.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.

10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu.

10. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao.

11. Thamani yako inategenezwa na watu wengine, wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao.

13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.

14. Kumbuka asili yako, kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.

15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia. Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.

Kumbuka: Ishi kwa kumpendeza Mungu.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki niย Soft copy [pdf]ย kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

[products columns="2" ids="30827"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kujenga Mfumo wa Ushirikiano katika Mambo ya Kifedha na mke wako

Jinsi ya Kujenga Mfumo wa Ushirikiano katika Mambo ya Kifedha na mke wako

Kujenga mfumo wa ushirikiano katika mambo ya kifedha na mke wako ni muhimu katika kudumisha ustawi n... Read More
Kujenga Ushirikiano wenye Uaminifu na Kujenga Imani katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Uaminifu na Kujenga Imani katika Familia

Kujenga Ushirikiano Wenye Uaminifu na Kujenga Imani katika Familia

Familia ni moja ya vitu... Read More

Kuhamasisha Kujitambua na Kujielewa katika Mahusiano

Kuhamasisha Kujitambua na Kujielewa katika Mahusiano

  1. Kujitambua na Kujielewa ni jambo muhimu sana katika mahusiano. Kujitambua kunamaanisha ... Read More

Kwa Wanaume: Mbinu za Kufanya Kazi vizuri na Kupata Mafanikio

Kwa Wanaume: Mbinu za Kufanya Kazi vizuri na Kupata Mafanikio

Read More
Je, umri unaathiri ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, umri unaathiri ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, umri unaathiri ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Hakuna jibu moja sahihi kwa swal... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ahisi Anapendwa na Kuthaminiwa

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ahisi Anapendwa na Kuthaminiwa

Habari za asubuhi wapendwa! Leo, tutajadili vidokezo muhimu ambavyo vitamsaidia msichana ahisi an... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za tabia na mienendo ya watoto wenu na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za tabia na mienendo ya watoto wenu na mpenzi wako

Kama wazazi na wenzi, tunajua kuwa kuna tofauti katika tabia na mienendo yetu. Lakini pia, inawez... Read More

Njia za Kuimarisha Uhusiano wa Kihisia na Kimahaba na mke wako

Njia za Kuimarisha Uhusiano wa Kihisia na Kimahaba na mke wako

Kuimarisha uhusiano wa kihisia na kimahaba na mke wako ni muhimu katika kudumisha ndoa yenye furaha ... Read More
Kukuza Urafiki na Upendo katika Familia Yako ili Iwe na Amani na Furaha

Kukuza Urafiki na Upendo katika Familia Yako ili Iwe na Amani na Furaha

Kufanya familia yako kuwa na upendo na amani inahitaji jitihada kutoka kwa kila mmoja. Ni muhimu ... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu maadili ya kifedha na matumizi

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu maadili ya kifedha na matumizi

Kuwa na mazungumzo kuhusu maadili ya kifedha na matumizi ndio jambo muhimu sana katika mahusiano.... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya hisia na utambuzi katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya hisia na utambuzi katika uhusiano wa ngono/kufanya mapenzi?

Habari rafiki yangu! Leo tuzungumzie suala muhimu sana ambalo linapaswa kujadiliwa katika uhusian... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na dini na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiimani na dini na mpenzi wako

Mapenzi ni hisia za kipekee ambazo huja na changamoto zake. Mojawapo ya changamoto kubwa katika u... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About