Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Wosia mzuri wa baba kwa mwanae

Featured Image

Mwanangu, mimi baba yako nimeishi miaka mingi kuliko wewe ndio maana unaniita baba. Ni kweli sijasoma kama wewe ulivyosoma Ila mambo niliyokutana nayo tangu nimezaliwa ni elimu tosha ambayo wewe huna. Sasa nataka nikupe Elimu hiyo ili ukijumlisha na elimu yako ya darasani ujue namna nzuri ya kuishi katika dunia hii iliyojaa mishangazo mingi.

Maisha ni jumla ya mambo yote unayoyatenda kila siku. Namaanisha kila unalolifanya Leo linaathiri maisha yako ya kesho kwa hali chanya au hali hasi. Na kama ni hali hasi ni kwa ukubwa gani halikadharika kama ni hali chanya ni kwa kiwango gani. Mwanangu kila jambo unalolifanya Leo huamua ni mlango gani Unaweza ingia Kesho lakini pia mlango upi huwezi ingia Kesho. Ndio maana ni muhimu kuijua Kesho yako ukiwa Leo.

Mwanangu ili ufanikiwe ni lazima ujue kuishi na watu vizuri. Na mimi sikushauri kabisa kwamba uwe na marafiki wengi. Kuwa na marafiki wengi ni moja ya eneo unaweza jitengenezea mtego mbaya wa kukuangamiza kesho yako. Mwenye hekima mmoja aliwahi kusema ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe. Mwanangu kwa kusema hivyo simaanishi uwe na maadui,hapana. Ila marafiki zako watakusaidia mlango unaotaka kuingia Kesho uingie kwa urahisi au kwa ugumu au usiingie kabisa na wakati mwingine Unaweza kuingia na wakahusika kukutoa kwa aibu kubwa. Ndio maana ni muhimu Kuwa na marafiki ila Kuwa nao wachache chagua kwa makini mno. Sio lazima kila akufaaye kwa dhiki ndiye awe rafiki. Kuna watu wanakufaa kwa dhiki Leo ila Kesho wakutumikishe Kuwa makini sana.

Mwanangu, kuwa makini sana na mahusiano yako ya kimapenzi maana yanagusa hisia zako na mtu unayehusiana naye moja kwa moja. Hivyo basi kuwa makini maana mahusiano hayo yanaweza kukufanya Kesho ukamkosesha raha utakayekuwa naye kama sio huyo uliyenaye leo ndie ukajaaliwa Kuwa naye Kesho. Mwanangu, Unaweza kuniona mshamba sababu ulimwengu wenu unaonekana kama haujali sana haya mambo ila tafadhari zingatia utakapofika Kesho utaelewa sana hiki ninachokuambia.

Mwanangu, jichunge sana na mambo unayoyafanya Leo na uwe muungwana na kupenda haki. Tamaa isikupeleke ukafanya mambo mabaya ambayo yatakulazimisha kutunza siri moyoni mwako hata kama utafika ile Kesho yako. Jiepushe kabisa na mambo mabaya ya siri ya nafsi. Hakuna utumwa mbaya kama utumwa ndani ya nafsi yako mwenyewe maana kila ukikumbuka nafsi itakusuta na kukukosesha raha ya kweli. Hivyo kubali na kuridhika na ulivyo kama huwezi kujiongeza kwa njia halali na za haki. Ni heri uwe masikini mwenye uhuru ndani kuliko uwe tajiri na maarufu mwenye siri mbaya ndani ya Moyo wako. Mwanangu tafadhari uwe makini sana.

Mwanangu, siwezi sahau kukwambia kuhusu Mungu. Maisha ya uchaji wa Mungu yatakuepusha na mengi. Hapa naomba unielewe kwamba usijifanye unamcha Mungu bali mche Mungu. Sio kwasababu unashida ya kufanikiwa ndio umche Mungu, hapana! Bali umche Mungu sababu ni Mungu na yeye ndiye anaijua Kesho yako vizuri kuliko wewe mwenyewe. Ukimshirikisha mambo yako na ukawa mwaminifu kwake hakika hatakuacha kamwe.

Mwanangu, usiku umeenda nenda kalale sasa ila usije ukapenda na kutamani waovu kwa uovu wao na wakakushawishi ujiunge nao. Tafadhari usikubali.

#Kizazi Ganzi#

JIFUNZE KUJIFUNZA

Mwl Makwaya
Kuwa Ni Kufanya.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki niย Soft copy [pdf]ย kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

[products columns="2" ids="30827"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuwa Mlezi Mzuri: Mbinu za Kulea Watoto Wanaojiamini na Wanaofaulu

Jinsi ya Kuwa Mlezi Mzuri: Mbinu za Kulea Watoto Wanaojiamini na Wanaofaulu

Kuwalea watoto si jambo rahisi wala halina changamoto zake. Kuwa mlezi mzuri ni kitu ambacho kila... Read More

Jinsi ya kujua kama mwanamke anakupenda kweli kwa dhati

Jinsi ya kujua kama mwanamke anakupenda kweli kwa dhati

Yafuatayo ni maswali ya kujiuliza ili kujua kama mwanamke anakupenda kweli.

Anajitoa kwa ... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mke wako katika Kutimiza Malengo ya Kibinafsi

Jinsi ya Kusaidiana na mke wako katika Kutimiza Malengo ya Kibinafsi

Kusaidiana na mke wako katika kutimiza malengo ya kibinafsi ni sehemu muhimu ya kuimarisha uhusiano ... Read More
Je, inafaa kuzungumzia kuhusu historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano?

Je, inafaa kuzungumzia kuhusu historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano?

Je, kuna haja ya kuzungumzia historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano? Jib... Read More

Kuweka Kipaumbele cha Kuendeleza Ushirikiano wa Kujenga katika Mahusiano

Kuweka Kipaumbele cha Kuendeleza Ushirikiano wa Kujenga katika Mahusiano

Kuweka Kipaumbele cha Kuendeleza Ushirikiano wa Kujenga katika Mahusiano

Kuwa na mahusiano... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano na Kujenga Upendo katika Familia Yako

Njia za Kuimarisha Ushirikiano na Kujenga Upendo katika Familia Yako

Familia ni kitovu cha upendo na ushirikiano. Ni mahali pa kujifunza na kukua kwa pamoja. Hata hiv... Read More

Jinsi Mwanamme Unavyoweza kubobea katika Mapenzi na Mahusiano

Jinsi Mwanamme Unavyoweza kubobea katika Mapenzi na Mahusiano

Read More
Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya kijamii na kujitolea

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya kijamii na kujitolea

Mawasiliano ndio msingi wa mahusiano yoyote ya kimapenzi. Kuwa na uwezo wa kuzungumza na mpenzi w... Read More

Jinsi ya Kuishi kwa Upendo na Kusaidiana katika Familia yako

Jinsi ya Kuishi kwa Upendo na Kusaidiana katika Familia yako

Karibu katika makala hii kuhusu jinsi ya kuishi kwa upendo na kusaidiana katika familia yako. Fam... Read More

Mbinu za Kupata Tarehe na Wasichana kwa Mafanikio

Mbinu za Kupata Tarehe na Wasichana kwa Mafanikio

Leo, tunazungumzia mbinu za kupata tarehe na wasichana kwa mafanikio. Kila mtu anataka kuwa na mp... Read More

Jinsi ya Kuimarisha imani na kuaminiana katika uhusiano na mpenzi wako

Jinsi ya Kuimarisha imani na kuaminiana katika uhusiano na mpenzi wako

Kuimarisha imani na kuaminiana katika uhusiano wako na mpenzi wako ni muhimu sana kwa kujenga uhusia... Read More
Kuhamasisha Ushirikiano wa Kielimu na Kuweka Mazingira ya Kujifunza katika Familia

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kielimu na Kuweka Mazingira ya Kujifunza katika Familia

Kuhamasisha Ushirikiano wa Kielimu na Kuweka Mazingira ya Kujifunza katika Familia

Elimu n... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About