Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Kupima lishe au afya ya mtu

Featured Image

Njia za kupima Afya

Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;

1. Vipimo vya umbile la mwili

2. Vipimo vya maabara

3. Kuchukua historia ya ulaji na maradhi

Vipimo vya umbile la mwili

Baadhi ya vipimo ambavyo vinaweza kutumika kutoa tahadhari kuhusu magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza ni;

1. Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).

2. Mzunguko wa kiuno.

3. Uwiano wa mzunguko wa kiuno na nyonga.

4. Kulinganisha uzito na umri.

Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).

Hiki ni kipimo kinachotumika kuangalia uwiano wa urefu na uzito wa mtu, ni muhimu kuchukua vipimo kwa usahihi.Uwiano wa uzito katika Kilogramu na urefu katika mita hupatikana kwa kutumia kanuni ifuatayo:

BMI= uzito (Kg)/Urefu2 (m2)

BMI huwa na viwango mbalimbali vilivyowekwa na shirika la Afya duniani (WHO) kutafsiri hali ya lishe ya mtu ambavyo ni

1. BMI chini ya 18.5 = uzito pungufu.

2. BMI kati ya 18.5 mpaka 24.9= uzito unaofaa.

3. BMI kati ya 25.0 mpaka 29.9 = unene uliozidi.

4. BMI ya 30 au zaidi = unene uliokithiri au kiribatumbo.

Mahitaji ya chakula mwilini hutegemea umri, jinsi, hali ya kifiziolojia (kama ujauzito na kunyonyesha), hali ya kiafya, kazi na mtindo wa maisha. Uzito wa mwili hutegemea na chakula unachokula, pamoja na shughuli unazofanya, mara nyingi unene hutokana na kula chakula kwa wingi.
Unene uliokithiri unachangia kwa kiwango kikubwa kupata magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza kama kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo kubwa la damu, na saratani. Uzito uliozidi unapaswa kupunguzwa ili kuepuka magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza

Jinsi ya kupunguza unene uliozidi

1. Tumia mafuta kwa kiasi kidogo kwenye chakula

2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi hususani vinavyopikwa kwa kudumbukizwa kwenye mafuta, au vinavyokaangwa kwa mafuta mengi.

3. Epuka matumizi ya vinywaji au vyakula venye sukari nyingi

4. Epuka asusa zenye mafuta mengi au sukari nyingi kati ya mlo na mlo.

5. Ongeza vyakula venye makapi- mlo kwa wingi kama matunda, mboga mboga na nafaka zisizokobolewa.

BMI haitumiki kwa wanawake wajawazito, BMI haitumiki kwa watoto na vijana walio na umri chini ya miaka 18, BMI haitumiki kwa watu wasioweza kusimama vyema, waliovimba miguu, na wanawake wanaonyonyesha katika miezi sita ya mwanzo baada ya kujifungua.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Ngogwe Na Bamia

Jinsi ya kupika Mchuzi Wa Ngogwe Na Bamia

Viamba upishi

Ngogwe ยฝ kg
Kitunguu 2
Bamia ยผ kg
Karoti 2
Mafuta vij... Read More

Mapishi ya Biskuti Za Jam

Mapishi ya Biskuti Za Jam

VIAMBAUPISHI

Unga 2 ยฝ gilasi

Sukari ยพ gilasi

Samli 1 gilasi

Mayai 2Read More

Mapishi ya Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Mapishi ya Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Mahitaji

Mchele - 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) - Mug

Tuna... Read More

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Karanga

Jinsi ya kuandaa Vileja Vya Karanga

MAHITAJI

Mayai 5

Sukari 450gm (1ย lb)

Unga wa Ngano 1ย kg

Siagi 450gm (... Read More

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora

Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora ๐ŸŽ๐Ÿฅฆ

Habari za leo wapendwa wasoma... Read More

Mapishi ya Mitai

Mapishi ya Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano - magi 2 (vikombe vikubwa)

Hamira kijiko 1 cha chai

<... Read More
Upishi na Maboga: Yenye Virutubisho na Ya Kuvutia

Upishi na Maboga: Yenye Virutubisho na Ya Kuvutia

Upishi na Maboga: Yenye Virutubisho na Ya Kuvutia ๐Ÿฅฆ๐Ÿฅ’๐Ÿฅ•

Habari za leo wapenzi wa up... Read More

Virutubishi, kazi zake katika mwili na vyanzo vyake

Virutubishi, kazi zake katika mwili na vyanzo vyake

Virutubishi

ni viini vilivyoko kwenye chakula ambavyo vinauwezesha mwili kufanya kazi zak... Read More

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako

Vitafunio vya Afya kwa Kutosheleza Hamu Zako ๐Ÿ‡๐ŸŽ๐Ÿฅ•

Hakuna jambo bora zaidi kama kuf... Read More

Jinsi ya kupika Wali wa hoho

Jinsi ya kupika Wali wa hoho

Wali wa hoho ni chakula maalum kinachotumika katika hafla au sherehe. Ni chakula chenye ladha nzu... Read More

Mapishi mazuri ya Chapati za maji

Mapishi mazuri ya Chapati za maji

Mahitaji

Unga wa ngano (plain flour) ( 1/4 kilo)
Yai (egg 1)
Sukari (sugar 1/4 ... Read More

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mapishi ya Bokoboko La Kuku

Mahitaji

Ngano nzima (shayiri) - 3 Vikombe

Kuku - ยฝ (3 LB takriban)

Thomu na... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About