Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

Mapishi ya Pilau Ya Bilingani Na Kuku

Featured Image

Viambaupishi

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Bilingani - 2 ya kiasi

Viazi - 4

Vitunguu - 2

Kitunguu (thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 2

Chumvi - kiasi

Garama masala (mchanganyiko wa bizari) - 1 kijiko cha chai

Hiliki ya unga - ¼ kijiko cha chai

Mafuta ya kupikia wali - ¼ kikombe

Mafuta ya kukaangia viazi na bilingani - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:

Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele.
Kata kuku vipande upendavyo safisha
Kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu, na bizari mchanganyiko (garama masala).
Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria.
Menya na kata viazi kaanga weka kando.
Kata kata bilingani slesi nene kaanga, chuja mafuta weka kando.
Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi. Tia vipande vya kuku, ukaange kidogo.
Tia supu ya kuku, mchele, tia hiliki, ufunike hadi karibu na kuwiva kabisa.
Tia viazi na bilingani uchanganye kidogo, kisha tia katika oven imalizike kupikika pilau humo au unaweza kuendelea kufunika juu ya jiko hadi pilau iwive.
Pakua katika sahani ikiwa tayari kuliwa kwa saladi ya mtindi.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Mapishi ya Wali Wa Mboga Na Samaki Wa Pink Salmon

Vipimo

Mchele 3 vikombe

Mboga mchanganyiko 1 kikombe

Samaki wa Pink Salmon 5 ... Read More

Mapishi ya Viazi vya nyama

Mapishi ya Viazi vya nyama

Mahitaji

Viazi (potato) 1 kilo
Nyama ya ng'ombe 1/2 kilo
Nyanya ya kopo iliyosa... Read More

Mapishi ya Wali, mchicha wa nazi na nyama ya kukaanga

Mapishi ya Wali, mchicha wa nazi na nyama ya kukaanga

Mahitaji

Mchele (rice 1/2 kilo)
Mchicha uliokatwakatwa (spinach mafungu 2)
Nyam... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu

Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu

MAHITAJI

Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2

... Read More

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Viambaupishi

Mchele 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu 1 Mug

(Frozen veg)Read More

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

1. Chakula

ni kitu chochote kinacholiwa au kunywewa na kuupatia mwili virutubishi mbalimb... Read More

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri 🥗🌿

Hakuna shak... Read More

Mapishi – Saladi ya Matunda

Mapishi – Saladi ya Matunda

Matunda ni mojawapo wa kundi la vyakula, ni muhimu sana kwa afya bora. Matunda yakitengenezwa viz... Read More

Mapishi ya Sambusa za nyama

Mapishi ya Sambusa za nyama

Mahitaji

Nyama ya kusaga (minced beef 1/4 kilo)
Vitunguu maji vilivyokatwakatwa(dice... Read More

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - ... Read More

MAPISHI YA LADU

MAPISHI YA LADU

VIAMBAUPISHI

Unga - 6 vikombe

Samli - ½kikombe

Baking Powder - ½kijiko cha ... Read More

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Mara nyingi biringanya hutumika kama kiungo cha nyongeza katika mchuzi. Hata hivyo, kiungo hiki k... Read More

📖 Explore More Articles
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About