Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/personal/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:

Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:

Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:

Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:

Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:

Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:

Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Mtu anaweza kurithi uvutaji wa bangi?

Hapana, huwezi ukarithi uvutaji wa bangi. Lakini mara nyingi watoto huiga tabia za wazazi wao. Wa... Read More

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za umri katika ngono/kufanya mapenzi? Ndio, kuna tofauti nyingi sana! Hiyo ndiyo... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ajiambie Kuwa Anakupenda

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ajiambie Kuwa Anakupenda

Kila mwanamume anapenda kujua kama msichana anayempenda anahisi hivyo hivyo kumhusu. Lakini sio k... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili masuala ya usalama na faragha katika ngono/kufanya mapenzi?

H... Read More

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Je, ni kweli kuwa ulemavu unaweza kugundulika mara tu mtoto anapozaliwa?

Ni kweli kuwa daktari anaweza kufanya vipimo vya kugundua
kama mtoto aliye tumboni ni mwenye... Read More

Je, mwanamke anaweza kufikia mshindo (kufika kileleni)?

Je, mwanamke anaweza kufikia mshindo (kufika kileleni)?

Ndiyo, mwanamke anaweza kufikia mshindo wakati wa kujamiiana. Dalili ya mwanamke kufikia mshindo ... Read More

Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

  1. Je, watu wanapenda kujaribu nafasi mpya za ngono/kufanya mapenzi?

Hivi karibu... Read More

Je, ni kweli kwamba mwanamke akikaa muda mrefu akiwa bikira ni shida sana kuvunja kizinda akijamiiana kwa mara ya kwanza?

Je, ni kweli kwamba mwanamke akikaa muda mrefu akiwa bikira ni shida sana kuvunja kizinda akijamiiana kwa mara ya kwanza?

Ile ngozi ndani ya uke i inabakia kuwa nyembamba na laini sana, hata mwanamke akiwa bikira katika... Read More

Je, kuna tofauti za kitamaduni katika mtazamo wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna tofauti za kitamaduni katika mtazamo wa ngono/kufanya mapenzi?

Habari za leo wapenzi wa Kiswahili! Leo tutajadili suala la tofauti za kitamaduni katika mtazamo ... Read More

Kwa nini Albino wanawekwa katika kundi la watu wenye ulemavu?

Kwa nini Albino wanawekwa katika kundi la watu wenye ulemavu?

Ulemavu maana yake ni hitilafu katika mwili au akili inayomwekea
mipaka mtu asiweze kufaniki... Read More

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu? πŸ€”

Jambo zuri kujiuliz... Read More

Jinsi ya Kutambua Ishara za Upendo kutoka kwa Msichana

Jinsi ya Kutambua Ishara za Upendo kutoka kwa Msichana

Upendo ni hisia ambazo zinafanya maisha kuwa na maana zaidi. Kila mtu anapaswa kupata upendo, na ... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About